Jumamosi, 19 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Kujitawala Wenyewe” kwa Mujibu wa Matakwa ya Wakoloni!

Ardhi zetu za Kiislamu zimekuwa jukwaa la kupigania mali na ushawishi kati ya Marekani na Ulaya. Cha kusikitisha ni kwamba, zana za mapambano haya ni baadhi ya wana wa Ummah, iwe katika serikali au vuguvugu la waasi, kama inavyotokea leo nchini Sudan, wakati wanaoshindwa pekee katika vita hivi ni watu wasio na hatia, wasio na nguvu.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mwanachama wa Afisi ya Amiri, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama)

Amiri wa Hizb ut Tahrir, Wanachama wa Afisi ya Amiri, Diwani ya Al-Madhalim (Malalamiko), na Afisi Kuu ya Habari na Hizb ut Tahrir kwa jumla wanaomboleza kwa Umma wa Kiislamu Mwanachama wa Afisi ya AmIrI, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama) aliyefariki dunia asubuhi ya leo, 22 Rabi’ Al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 14 Septemba 2025 M, akiwa na umri wa miaka themanini na saba.

Soma zaidi...

Mateso ya watu wa Palestina kwenye Daraja la Mfalme Hussein (Allenby) Kati ya Msongamano, Ufisadi, na Mfumo wa Hatari wa Tabaka la VIP

Kwa kuzingatia njama ya dola jirani  za eneo dhidi ya Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ili kukaza mzingiro dhidi ya watu wake, kuwadhuru, na kuwasukuma kuiacha ardhi yao na kuikabidhi kwa Mayahudi, Daraja la Mfalme Hussein (Allenby au Karameh) linaunda njia kuu ya maisha ya watu wa Palestina kwa ulimwengu wa nje. Hata hivyo, kivuko hiki, ambacho kinapaswa kuwa njia ya usafiri, kimekuwa chanzo cha mateso ya kila siku kwa wasafiri, hasa upande wa Jordan, ambapo mambo ya kibinadamu, ya kiutawala, na ya kisiasa yanaingiliana na kuunda mandhari katili sana.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Jordan na Wanajeshi Wake: Jihadharini na Kundi la Kitengo cha Gilead, Vitisho vya Umbile la Kiyahudi kwa Nchi yenu, na Ushiriki na Utiifu wa Serikali!

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Ziara ya Ujumbe wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Lebanon kwa Mufti wa Sidon na Wilaya zake

Katika muktadha wa mawasiliano na wanasiasa, wanajamii wa Kiislamu huko Sidon, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Wilayah Lebanon ukiongozwa na Hajj Ali Aslan, Mwanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Mhandisi Bilal Zaidan, Mwanachama wa Kamati ya Shughuli na Hajj Hassan Nahlas, Mkuu wa Kituo cha Sidon, walimtembelea Mheshimiwa Mufti wa Sidon na wilayah zake, Sheikh Salim Sosan.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan - mbele ya Msikiti Mkuu jijini Port Sudan Wito kwa Watu wa Sudan... Msiiruhusu Amerika Kuichana Nchi Yenu na Kuivua Darfur

Enyi Waislamu: Mataifa katika maisha yao yana masuala nyeti, yaani, masuala ambayo mtu anakuwa na msimamo mmoja: yhai chini yao au kifo kwao. Itikadi ya Uislamu imetubainishia sisi Waislamu masuala yetu nyeti; yaani yale ambayo kipimo chake ni uhai au kifo. Miongoni mwa masuala hayo nyeti ni suala la umoja wa dola na umoja wa Ummah. Tulipoondoa suala hili kwenye kituo chake stahiki hapo awali, Amerika, kwa msaada wa baadhi ya watu wetu, iliweza kuichana nchi yetu na kuitenganisha Sudan Kusini, na sasa inaregea kukamilisha kile ilichoanza mwanzo kuchora, kwa mipaka ya damu, dola mpya katika mabaki ya nchi yetu; kwa kuivua Darfur, ambako matukio yanazidi kupamba moto katika kutumikia njama ya Amerika kwa usaidizi wa zana zake ndani na nje.

Soma zaidi...

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa kutenganisha Darfur, Hizb ilifanya Visimamo katika miji kadhaa ya Sudan

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa Marekani wa kuichana nchi hii kwa kuitenganisha Darfur na Sudan, hizb ilifanya kisimamo katika Msikiti wa Al-Aqit mjini Gadharef mnamo siku ya Alhamisi, Septemba 11, 2025 baada ya swala ya Ijumaa Septemba 12, 2025, miji kadhaa mikubwa ya Sudan ilifanyika visimamo, pamoja na misikiti mikuu ya Sudan yote. Shawak, Singa, Rabak, Madani, Abbasiya, Taqli, Khartoum (Kalakila na Dukhainat), na misikiti miwili mjini Omdurman.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Sudan Wilayah – Mji wa Kosti, Jimbo la White Nile Wakutana na Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party katika Jimbo la White Nile

Mnamo Ijumaa, 12 Septemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilaya ya Sudan ulimtembelea Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party, katika Uwanja wa Azraq Taiba huko Kosti.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu