Machozi ya Furaha kwa Maadui wa Mwenyezi Mungu, Kushindwa na Kukata Tamaa kwa Waislamu nchini Cyprus
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Aprili iliyopita, Baraza la Mawaziri la Cyprus Kaskazini lilitoa “amri ya kiserikali” ambayo inaruhusu wanafunzi kuvaa hijabu za Kiislamu katika shule za sekondari. Hata hivyo, Muungano wa Walimu wa Sekondari wa Cyprus na Uturuki (KTOEOS), ulianza migomo, ukakataa kufundisha watoto waliofika shuleni wakiwa wamevalia mavazi ya kidini, na hatimaye wakaiomba Mahakama Upeo. Wiki iliyopita (mwisho wa Septemba), Mahakama ya Upeo ya Cyprus Kaskazini ilibatilisha “amri ya kiserikali”, ikiamua kuwa ilikuwa kinyume na katiba. Viongozi wa Muungano huo wa Walimu, ambao waliomba kubatilishwa kwa amri hiyo, walisherehekea kuregea kwa marufuku ya hijabu kama “ushindi kwa usekula” kwa kububujika “machozi ya furaha”. Wakati huo huo serikali imetangaza kuanza mara moja “kufanyia kazi sheria mpya”.



